Mgombea urais CHAUMMA akabidhiwa zawadi na wananchi wa Mombo

By Elizabeth Zaya , Nipashe
Published at 11:45 AM Sep 04 2025
Mgombea urais wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu.
Picha: Elizabeth Zaya
Mgombea urais wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu.

Mgombea urais wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, amepokea zawadi kutoka kwa wananchi wa Mombo, jimbo la Korogwe Vijijini, mara baada ya kumaliza kuzungumza nao katika mkutano wa hadhara.

Wananchi hao walimkabidhi zawadi hizo kama ishara ya upendo na kuonesha mshikamano wao naye, wakati akiendelea na ziara ya kampeni katika mikoa ya Kaskazini.