Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi, amesema amemtembelea hospitalini Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Dk. Charles Kitima, na kumfikishia ujumbe wa watanzania wapenda haki.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mwabukusi ameandika:
"Nimemtembelea Father Dr. Charles Kitima. Hakika lilikuwa shambulio baya lenye lengo la kudhulumu maisha."
Ameongeza kuwa hali ya Padri Kitima inaendelea vizuri, na kwamba Mungu ni mwema. Aidha, ametoa ujumbe alioueleza kuwa umetoka kwa Padri Kitima mwenyewe kwa ajili ya watanzania wote. Ujumbe huo unasema:
Padri Kitima alishambuliwa Aprili 30, 2025, majira ya saa nne usiku, mara baada ya kutoka katika eneo alilokuwa akipata kinywaji. Alipokuwa akielekea maliwatoni, alishambuliwa kwa kupigwa na kitu butu kichwani.
Taarifa ya Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ya Mei 1, 2025, imeeleza kuwa mtu mmoja anashikiliwa kwa tuhuma za kuhusika na shambulio hilo dhidi ya Padri Kitima.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED