Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan, ameahidi kufufua viwanda vya kubangua korosho katika wilaya ya Tunduru, mkoani Ruvuma, akisema ndiyo maana serikali imeleta umeme wa kutosha katika eneo hilo.
Akizungumza leo, Septemba 22, 2025, na wananchi wa Tunduru, lenye majimbo mawili ya Kusini na Kaskazini, Samia amejinadi na kutoa ahadi hiyo huku akisisitiza kuwa Serikali yake itahakikisha maendeleo ya kiuchumi ya wilaya hiyo.
“Kuna vitalu 221 vinasubiri kutumiwa na wafugaji; baadhi vimekwisha kutumika na vingine bado tutaleta wawekezaji ili vikuze uchumi wa Wilaya hii,” amesema Samia.
Aidha, ameahidi:
Aidha, Samia amesema Serikali yake itachukulia kwa makini maombi ya halmashauri yaliyowasilishwa na mgombea ubunge wa eneo hilo, akiahidi kuyachakata na kuona ni yapi yatakayotekelezwa kwanza.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED