Samia aahidi kukamilisha machinjio ya kisasa Mbeya

By Romana Mallya , Nipashe
Published at 06:53 PM Sep 04 2025
Samia aahidi kukamilisha machinjio ya kisasa Mbeya
Picha: CCM
Samia aahidi kukamilisha machinjio ya kisasa Mbeya

Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),Samia Suluhu Hassan, ameahidi wananchi wa Mkoa wa Mbeya kuwa, endapo atapata ridhaa nyingine kuongoza nchi, kukamilisha ujenzi wa machinjio ya kisasa yaliyoko katika eneo Utengule mkoani humo.

Samia ametoa ahadi hizo leo Septemba 4, 2025, katika mkutano wa kampeni wa  CCM wilayani Mbalali, mkoani Mbeya.

Dk. Samia ametoa wito kwa wafugaji kuendelea kushiriki katika kampeni ya chanjo ya mifugo na utambuzi wa mifugo yao inayoendelea nchi nzima, ili  kuzalisha nyama yenye viwango vya kimataifa ambayo ina soko kubwa kimataifa.

Amewaeleza kuwa huko nyuma walikuwa wanakosa soko kwa sababu walikuwa hawana rekodi na hawachanjwi.

Amesema wameanzisha huduma ya kuchanja na kuwatambua kwa kuwa soko la nyama nje ya nchi ni kubwa, akiwataka waendelee kufuga, ili wauze nyama na wanyama hai nje.