Mgombea wa urais kwa tiketi ya National League for Democracy (NLD), Doyo Hassan Doyo, amezindua kampeni yake ya kitaifa jijini Tanga na kutaja misingi sita itakayokuwa msingi wa uongozi wa chama hicho endapo kitapata ridhaa ya wananchi kuingia Ikulu.
Doyo amesema kwamba NLD haikubahatishi kuingia madarakani, bali imejipanga na mikakati madhubuti ya kuongoza taifa, huku dira yake ikiwa ni kujenga Tanzania yenye maendeleo jumuishi.
“Maendeleo jumuishi yenye uchumi imara unategemea uzalishaji wa ndani, haki, ustawi na usawa wa kila Mtanzania. Ili kufanikisha dira hii, NLD litaongozwa na misingi mikuu sita,” amesema Doyo.
Misingi hiyo sita ni:
Aidha, Doyo ameahidi kwamba endapo atapata ridhaa ya wananchi, atahakikisha changamoto zote zitatatuliwa na uchumi unainuliwa ili wananchi wote, hasa walioko kwenye umasikini licha ya utajiri wa taifa, waweza kunufaika.
“Nchi yetu siyo masikini, lakini sisi tunaitwa wanyonge. Sasa ili msiitwe wanyonge, msifanye mchezo, changamkeni Oktoba 29, nendeni mnichague Doyo Hassan Doyo. Nitakwenda kubadilisha kila penye changamoto,” alisema Doyo.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED