PSSSF yaongeza nguvu mbio maalum kusherehekea miaka 61 ya muungano

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 08:59 PM Apr 26 2025
 PSSSF yaongeza nguvu mbio maalum kusherehekea miaka 61 ya muungano
Picha: Mpigapicha
PSSSF yaongeza nguvu mbio maalum kusherehekea miaka 61 ya muungano

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umedhamini mbio Maalum kusherehekea kilele cha miaka 61 ya Muungano wa Tanzania, hapa mkoani Singida

Mbio hizo za kilomita 10 na killomita 5 ziliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Singida, Martha Mlata, Wakuu wa Wilaya, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Hery Mkunda, Wafanyakazi wanaoshiriki Maonesho kuelekea Kilele cha Mei Mosi na Wananchi.

Mbio hizo zilifanyika katika Viwanja vya Chuo cha VETA.

 Akizungumza katika tukio hilo, RC Dendego alisema, "Ninawapongeza washiriki wote wa mbio hizi, tumepata bahati mbio hizi zinafanyika katika wiki ya kuelekea kilele cha sherehe za Mei Mosi ambazo kitaifa zitafanyika hapa mkoani Singida, lakini pia Mbio hizi zinaenzi miaka 61 ya Muungano wetu.”