'Tanga yafurahia msaada wa kisheria'

By Hamida Kamchalla , Nipashe
Published at 07:02 PM Apr 09 2025
'Tanga yafurahia msaada wa kisheria'
Picha: Hamida Kamchala
'Tanga yafurahia msaada wa kisheria'

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdallah, amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa Kampeni ya msaada wa kisheria kuwafikia wananchi wa Mkoa wa Tanga hatua ambayo itawezesha kupata Suluhu ya changamoto zao.

Ustaadh Abdallah amewasilisha shukrani hizo kwenye Viwanja vya Tangamano jijini, Tanga na kusema licha ya Kampeni hiyo kufika maeneo mbalimbali nchini wananchi wa Tanga walisubiri kwa hamu kufikiwa na huduma hiyo.

'Tanga yafurahia msaada wa kisheria'
"Tunamshukuru Rais kwa jambo hili kubwa lililofanyika maeneo mengi nchini, Tanga tulikuwa tukisubiri kwa hamu" amesema.
'Tanga yafurahia msaada wa kisheria'
Aidha amesema kwamba, lengo la kutolewa kwa huduma hiyo ni kuwezesha mtanzania masikini kupata msaada wa huduma za kisheria huduma ambayo inaotokewa baada ya serikali kugharimia.