Wateja 14 wa TANESCO wakatiwa huduma kisa kuhujumu miundombinu

By Ida Mushi , Nipashe
Published at 05:22 PM Sep 03 2025
Wateja 14 wa TANESCO wakatiwa huduma kisa kuhujumu miundombinu
Picha: Mpigapicha Wetu
Wateja 14 wa TANESCO wakatiwa huduma kisa kuhujumu miundombinu

Wateja 14 wa Shirika la Umeme nchini TANESCO Mkoa wa Morogoro wamesitishiwa huduma ya umeme baada ya kubainika wakitumia miundombinu ya shirika hilo kinyume cha sheria.

Mhandisi Mkuu wa TANESCO, ukanda wa Morogoro Kaskazini,Mhandisi Adam Abdula, amesema zoezi hilo litaendelea kuhakikisha mali za umma zinalindwa.

Miongoni mwa waliokamatwa ni Salim Ally,mkazi wa Kijiji cha Madudu wilayani Kilosa mfanyabiashara wa mashine za kusaga, aliyedaiwa kutumia umeme kwa kujiunganishia nyaya bila kufuata utaratibu rasmi wa TANESCO.

Wananchi wakiwemo viongozi wa vijiji  na mitaa katika wilaya za Kilosa, Morogoro Manispaa na Mvomero wamepongeza hatua hiyo ya Serikali  kupitia TANESCO wakisema itasaidia kudhibiti wizi wa umeme na kulinda miundombinu ya shirika hilo.