Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC ) imesema inashirikiana na jumuiya mbalimbali za kimataifa ili kulinda anga mtandao na madhara kwa wananchi.
Akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi na wahariri wa vyombo vya habari Jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa Usajili na Uzingatiaji wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC), Stephen Wangwe amesema kutokana na kila nchi kuwa na utaratibu wake katika masuala ya mtandaoni wameamua kubuni ushirikiano.
"Kuna kitu kinaitwa anga ya kimtandao ambayo haina mipaka ya kijiografia na kulikuwa na changamoto ya usimamizi wake kumekuwa na uhitaji wa kuwa na Sheria zinazofanana katika nchi zote"
"SADC wametengeneza Sheria za mfano zinazotakiwa kutumiwa na nchi wanachama ili kuwe na usimamizi unaofanana katika masuala ya mtandao kwa lengo la kulinda anga ya mtandao" amesema Wangwe.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED