RC Malima amwona mshindi Nanenane mleta mageuzi kwenye kilimo

By Christina Haule , Nipashe
Published at 04:51 PM Aug 05 2025
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima (kushoto), akipokea zawadi ya tunda la Bitroot kutoka kwa Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, SACP Peter Anatory (mwenye suti), mara baada ya kutembelea banda la Magereza
Picha; Christina Haule
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima (kushoto), akipokea zawadi ya tunda la Bitroot kutoka kwa Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza, SACP Peter Anatory (mwenye suti), mara baada ya kutembelea banda la Magereza

MKUU wa Mkoa wa Morogoro Adam Kighoma Malima amesema mshindi wa maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki, atapatikana kutokana na bidhaa anazoonesha uwanjani na shamba darasa analoendeleza kwa wakulima eneo alikotoka.

Malima amesema hayo leo, wakati alipotembelea maonesho hayo yanayofanyika kwenye uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere, uliopo eneo la Tungi, nje kidogo ya manispaa ya Morogoro. 

Amesema wakulima wameonekana kuitikia hasa katika upande wa mazao ya vipando na kutoa elimu kwa wakulima, jambo ambalo wanapaswa kulifanya kwa kuweka mashamba darasa kwenye maeneo wanakotoka, ili kuleta mageuzi yanayotakiwa kwenye kilimo nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima, (wa nne kutoka kulia), akimwaga chakula cha samaki kwenye bwawa la samaki lililopo katika banda la Magereza.
Hivyo amesema, ili kuleta chachu ya kilimo na maana ya maonesho hayo katika mwaka huu, watahakikisha washindi wanatokana na walichoonesha uwanjani na kwenye maeneo yao.