Vijana 400 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamekutana jijini Dar es Salaam kwa ajili ya uzinduzi wa Ilani ya Vijana 2025/2030, yenye lengo la kuongeza ushiriki wa kundi hilo katika maendeleo ya taifa, utawala bora wa kidemokrasia, amani na ustawi wa kijamii.
Uzinduzi huo umefanyika leo, Agosti 11, 2025, katika Makumbusho ya Taifa, ukiongozwa na Mwakilishi wa Ajenda ya Vijana, Joseph Malekela, ambaye alisema ilani hiyo inabeba matamanio, ndoto na mahitaji ya vijana katika nyanja mbalimbali.
Malekela ametaja nguzo kuu tano za kipaumbele zilizomo kwenye ilani hiyo kuwa ni:
Ameongeza kuwa ilani hiyo inataka kuwepo mkataba wa kijamii kati ya vijana na viongozi, ikiwasihi vyama vya siasa, watunga sera na taasisi kuingiza vipaumbele hivyo katika mipango yao.
Kwa upande wake, Mratibu wa Ajenda ya Vijana, Ocheck Msuya, amesema hatua hiyo inalenga kutoa vipaumbele na matarajio bayana, huku ikizingatia mahitaji ya makundi maalum. Pia alibainisha kuwa ilani hiyo imeandikwa kwa mfumo wa nukta nundu ili kuwawezesha watu wenye ulemavu wa kuona kuisoma.
Neema Divyele, Katibu wa Watu Wenye Ulemavu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni, ameitaka serikali kuweka mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu na kuwapa kipaumbele wakati wa kupiga kura.
Naye Elisha Luambano amesisitiza umuhimu wa kuzingatia mahitaji ya vijana katika nafasi mbalimbali za maamuzi, ili kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED