WANANCHI wa Kata ya Igwamanoni, Halmashauri ya Ushetu, mkoani Shinyanga, wamechangishana fedha zaidi ya Sh. milioni 10 kujenga upya shule ya msingi Igwamanoni iliyotitia.
Shule hiyo baadhi ya madarasa, baada ya mvua kubwa kunyesha Machi, mwaka jana yalititia, huku halmashauri ikiwaunga mkono kwa fedha za mapato ya ndani Sh. milioni 140.
Shule hiyo ilianzishwa mwaka 1983, ikiwa na vyumba saba vya madarasa na ofisi mbili za walimu, pamoja na matundu ya vyoo 12 na sasa inajumla ya wanafunzi 423 kuanzia darasa la kwanza hadi la saba.
Amesema, Machi 12, mwaka jana, majengo ya shule hiyo yalipata nyufa, baada ya mvua kunyesha kwa muda mrefu na kusababisha baadhi ya madarasa kutitia na kuhatarisha usalama wa wanafunzi, hali iliyowafanya wazazi na walezi kuchangisha fedha na kujenga shule mpya katika kijiji cha Iramba.
"Tunawapongeza wazazi na walenzi kwa kuchukua hatua za haraka kukabiliana na changamoto hii na sas ujenzi wake uko katika hatua ya mwisho kukamilika, wanafunzi bado wanaendelea na masomo yao katika vyumba vya madarasa vya sekondari ya Igwamanoni, walipohamishiwa baada ya tatizo hili kutokea," ameongeza Lema.
Mmoja wa wakazi wa Igwamanoni, Jumanne Kulwa, amesema walianzisha ujenzi wake kwa awamu 74 za mawe, mchanga 120 pamoja na kokoto awamu mbili, vikiwa na gharama ya zaidi ya Sh. milioni 10 na walifurahishwa zaidi baada ya serikali kuwaunga mkono.
Pia amewapongeza wazazi na walezi, kwa kujitolea kuanzisha ujenzi wa shule upya, kwa kuchangishana fedha na mahitaji mengine.
“Dhamira ya serikali inalenga kuboresha sekta ya elimu, ili kuhakikish wanafunzi wanasoma katika mazingira bora na kila mwaka bajeti ya wizara sekta hii, imezidi kuimarika zaidi.”
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED