ASKOFU wa Jimbo Katoliki Ifakara, Mhashamu Sulutaris Libana, amewataka watanzania kudumisha amani na kuzingatia makubaliano na maelewano, kwa kuwa ndiyo msingi wa amani.
"Sisi kama nchi tunafurahia amani, tunasema tuna amani na ni kweli, tuna amani kwani hatuna vita hatuna magomvi, amani iendane na upendo, iwe zao la ukweli na amani inatokana na upendo, amani inahitaji sana makubaliano na maelewano," amesema Askofu Libana.
Askofu Libana ameyasema hayo leo, Aprili 20, 2025, alipokuwa akitoa mahubiri wakati wa ibada ya Pasaka kitaifa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Andrea Mtume, Jimbo Katoliki lililopo Ifakara, mkoani Morogoro.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED