Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dk. Jim Yonazi, amesema kuwa Tanzania iko tayari kwa ajili ya kuandaa Mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), yanayotarajiwa kuanza rasmi Agosti 2, mwaka huu.
Akizungumza jana baada ya kufanya ziara ya ukaguzi wa miundombinu ya michezo jijini Dar es Salaam, Dk. Yonazi amesema maandalizi yamefikia hatua nzuri na viwanja viko tayari kwa mashindano hayo makubwa Afrika.
Dk. Yonazi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Makatibu Wakuu ya CHAN na AFCON, amekagua viwanja vya Benjamin Mkapa, Isamuhyo, Shule ya Sheria na Gymkhana.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, ametoa wito kwa Watanzania kuonesha uzalendo kwa kujitokeza kwa wingi viwanjani kuishangilia timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED