Part 3 : Walimu, wanafunzi wanavyo mzungumzia aliyetengeneza ‘A’ 100 za hisabati sekondari

By Halfani Chusi , Nipashe
Published at 01:07 PM Sep 01 2025
Part 3 : Walimu, wanafunzi wanavyo mzungumzia mwalimu aliyetengeneza ‘A’100 za hisabati sekondari

Bernard Mwakajila, muhitimu wa kidato cha sita aliyeshindwa kujiunga na chuo cha ualimu kutokana na ukosefu wa ada, ameibua mwanga mpya katika somo la hisabati kupitia shule ya Sekondari Kimara, Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam. Juhudi zake za kujitolea kufundisha zimetoa matokeo makubwa, ambapo wanafunzi wamepata ‘A’ 100 katika mtihani huo unaoogopewa na wengi.