Tume Umwagiliaji kujenga uzio na bwawa jipya

By Ida Mushi , Nipashe
Published at 05:52 PM Aug 30 2025
Tume Umwagiliaji kujenga uzio na bwawa jipya
PICHA: IDA MUSHI
Tume Umwagiliaji kujenga uzio na bwawa jipya

TUME ya Taifa ya Umwagiliaji inatarajia kujenga uzio na bwawa jipya katika shamba la umwagiliaji Dakawa, mkoani Morogoro. Hatua hiyo inalenga kulinda miundombinu, kuongeza tija ya kilimo na kuhakikisha wakulima wanapata maji ya uhakika kwa msimu wote.

Meneja wa Tume hiyo mkoani Morogoro, Mhandisi Juma Matanga, amesema mradi huo utasaidia pia kupunguza migogoro baina ya wakulima na wafugaji kutokana na mifugo kuharibu mazao na skimu za umwagiliaji. 

1

Naye Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Tume hiyo, Maria Itembe, amesema Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi katika miradi ya umwagiliaji kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa chakula cha kutosha na cha kuuza nje ya nchi.
2
Skimu ya Dakawa ina zaidi ya hekta elfu tatu zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji, huku hekta elfu mbili zikiwa zinatumika kwa sasa ambalo wafanyakazi wapya wa tume ya Taifa ya umwagiliaji wametembelea kujionea shughuli mbalimbali zinazofanyika.