Azzan ajitosa tena Kinondoni

By Beatrice Shayo , Nipashe
Published at 12:30 PM Jun 29 2025
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan
PICHA: BEATRICE SHAYO
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan

Aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan, amechukua fomu kugombea jimbo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam baada ya kuchukua fomu kinondoni amesema amerudi tena Kugombea Kwa lengo la kuwatumikia wananchi wa Jimbo hilo.

"Nimechukua fomu kama nitachaguliwa ndani ya chama kuwaongoza wananchi wa jimbo hili basi nitaongoza kwa kufuata utaratibu na kutekeleza ilani chama",amesema.

Azzan aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni kuanzia  2005 hadi 2015 kupitia Chama Cha Mapnduzi(CCM) kabla ya kuangushwa na Maulid Mtulia kupitia Chama Cha Wananchi (CUF).